Kashushura Awapongeza Waganga Wafawidhi Ukusanyaji wa Mapato

Adimin
0

Na Stephano Mango, Mbinga 

MKURUGENZI Joseph Kashushura amewapongeza   Waganga Wafawidhi wa vituo ya kutolea huduma za afya vilivyopo   Halmashauri  ya Wilaya ya Mbinga  kwa kuimarisha  usimamizi katika vyanzo vya mapato  ya ndani katika vituo  hatua iliyopelekea kuongezeka kwa mapato na upatikanaji wa huduma za afya.



Pongezi hizo zimetolewa jana katika Kikao cha kutoa tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe  katika kipindi cha robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2024/2025.


Baadhi ya viongozi hao  ambao wamepongezwa ni Mganga Mfawidhi Zahanati ya Myau  Amiri Kahurananga ambapo makusanyo ya kituo  yameongezeka kutoka 822,236.25 hadi kufikia 5,074,321 sawa na 


Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Halmashauri  ya Wilaya ya Mbinga Dkt. Salum Bundala ambapo makusanyo katika Hospitali hiyo yameongezeka kutoka 32,625,000 hadi kufikia 155,177,937 sawa na 373%.


Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya  Amani Makolo Joseph Washawasha, makusanyo yameongezeka kutoka  1,811,516.41  hadi kufikia  3,933,417.00 sawa na 217.13%.


Pamoja na pongezi hizo Mkurugenzi Kashushura amewataka Waganga Wafawidhi kuendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato katika vituo  wanavyovisimamia ili fedha  inayopatikana itumike katika  kuimarisha utoaji wa huduma bora  za afya kwa jamii.


Akizungumza kwa niaba ya washiriki hao Joseph Washawasha amebainisha kuwa  mafanikio hayo yametokana na kujituma,uzalendo pamoja na kutimiza majukumu yao kikamilifu.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top