DC Kasilda Afunga Mafunzo ya Mgambo Same,Wahitimu watakiwa kulitumikia Taifa

Adimin
0

Na Linda AKyoo 

Vijana askari 80 wa Jeshi la Akiba (Mgambo) wamehitimu mafunzo yao ya miezi minne yaliyofanyika katika kata ya Bombo, Tarafa ya Gonja Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro, askari hao wamekula kiapo cha utii kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,tayari kufanya kazi kwa kujitolea kulitumikia Taifa kama walinzi wa usalama wa raia na mali zao.


Akihitimisha mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Same Kasilda Mgeni amawataka kutumia mbinu walizofundishwa kwa manufaa ya jamii, hususani kulinda raia na mali zao, kuzingatia matumizi sahihi ya Silaha Pamoja na mbinu mbalimbali walizojifunza na kuepuka kujihusisha na matukio ya uhalifu.


Aidha amewasisitiza askari hao kwamba Pamoja na wajibu wao wa msingi kwnye masuala ya usalama, askari hao ni kiungo muhimu kuhamasisha uzalendo kwenye jamii, kuunganisha Serikali na jamii hasa panapohitajika ushiriki wa raia katika shughuli za kijamii za kujitolea Pamoja na kuchangia miradi ya maendeleo hasa nguvu kazi.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top