Tamasha la Kula Mbuzi Choma Makete Kufanyika Usiku wa Mkesha 'Mwaka Mpya 2025'

Adimin
0

 Kwa mara Nyingine Makete inaenda kuandika historia nyingine baada ya kuandaliwa kwa Tamasha la Mbuzi Choma ambalo litawahusisha wananchi wote watakaofika eneo la Soko la Ngiu Makete Mjini Kula Nyama kwa Uwezo wako bila Kulipia chochote.


Akizungumza Mratibu wa Tamasha hilo lililopewa jina la FUNGA MWAKA NA MBUZI CHOMA MAKETE 2024 Award Mpandila amesema lengo kuu ni Kuwahamasisha wananchi wa Makete Kupenda kurejea nyumbani, Kuoneshana Upendo ,kubadilishana mawazo ya maendeleo na kufahamiana kwa lengo la Kuijenga Wilaya ya Makete yenye Maendeleo.

Amesema Kwenye siku ya Disemba 31,2024 kunatarajiwa kuchinjwa Mbuzi 16 na kwa wale ambao hawali mbuzi basi wameandaliwa kondoo na kuku ambapo mpaka Disemba 29 2024 maandalizi yamekamilika kwa asilimia 90%. 


Endelea kufuatilia Idawa Media kwa Updates Zaidi kuhusu Tamasha la Kula Mbuzi Choma Makete 2024 RUDI NYUMBANI KUMENOGA.



Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top