Kizaazaa CCM Meru: Wanachama Wamrudishia Mgombea Sabuni, Sukari na Mahindi kwa Tuhuma za Rushwa"

Adimin
0

 BAADHI ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Ambureni Jimbo la Meru Wilayani Arumeru mkoani Arusha ambao ni mabalozi wa nyumba kumi na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kata wamerudisha katika ofisi ya chama kata hiyo vyakula na mali walivyopewa na mgombea udiwani wa kata kwa madai kuwa hiyo ni rushwa ambayo chama kinapinga mgombea kutoa katika kipindi cha uchaguzi.


Wanachama hao wamefikia uamuzi kurudisha ofisi Kata ya Ambureni baada ya mgombea huyo, Faraja Maliaki kugoma kufungua geti nyumbani kwake walipokwenda kupeleka vyakula kama mchele, mahindi, unga, sabuni, sukari na chumvi ili viongozi wa kata waweze kumkabidhi.

Mmoja wa wanaCCM aliyejitambulisha kwa jina la Eliaki Edward amesema viongozi wa chama ngazi za juu wamekuwa wakisisitiza wagombea kuacha kutoa rushwa kwa wajumbe wa kata na wilaya katika kipindi cha uchaguzi lakini wamekuwa wakipuuza maagizo hatua inayofanya wasiokuwa na fedha na mali kushindwa kupata uongozi na kuwapa mwanya wenye uwezo wa kifedha na mali kupita kwa ushawishi.

Bofya kusoma zaidi Read More

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top