DUWASA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI, KWENYE WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

Adimin
0

 Na Linda Akyoo ;Dodoma.

Ikiwa ni Muendelezo wa Wiki ya Huduma kwa wateja ,Mamlaka Ya maji safi na Usafi wa mazingira dodoma (DUWASA) Wamefika katika Mtaa wa Mlimwa C Uliopo  Jijini Dodoma Leo tarehe 08 Oktoba,2024 Kuwasikiliza wananchi na wateja wa mtaa huo,Ambapo wametoa malalamiko mbalimbali ikiwa ni pamoja na  kutopata maji kwa wakati na kuingiziwa bili ilihali hawapati huduma ya maji

Akijibu malalamiko ya wateja hao Mkurungezi wa huduma kwa wateja Duwasa  Bi Lena Mwakisale Amesema Suala la kusomewa Bili ya maji kwa wateja ni la Kila mwezi na Haki ya mteja kushirikishwa wakati wa usomaji wa Mita ya maji


Aidha Bi.Mwakisale Ameongeza kwa kuwaomba wananchi pindi wanapopata ujumbe wa Bili wakasome kwenye Mita zao ili kujua kama Bili iliyotumwa inauhalisia


Sambamba na hilo asema Kuwa Duwasa inatambua changamoto hiyo ya upungufu wa maji na wapo katika hatua nzuri ya kuhakikisha wananchi wa mtaa wa Mlimwa C wanaunganishwa kwenye bomba kubwa lililopo maeneo ya wajenzi.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top