Ondoeni Hofu kuhusu watoto hawa 200 kupata ufadhili wa Malezi kwa miaka 22

Adimin
0

 Na; Henrick Idawa

Wazazi na walezi wa watoto walisajiliwa na kufadhiliwa na shirika la compassion International Tanzania kupitia kanisa la TAG Tandala la wilayani Makete Mkoani Njombe wametakiwa kuondokana na dhana potofu juu ya ufadhili huo kwamba unaweza kupelekea watoto kufundishwa maadili mabaya.


Akitoa elimu ya ufadhili huo kwa wazazi na walezi Mratibu wa Mradi wa makuzi na malezi kwa watoto na vijana Isaack Philipo amesema lengo kuu ni kuwalea watoto hao kwa muda wa miaka 22 katika malezi kimwili,kiroho kiuchumi na kijamii ili kuandaa kizazi bora na si vinginevyo.

Amesema Mradi huo unalenga Zaidi kwenye suala la ulinzi na usalamaa la mtoto hivyo wazazi waendelee kuwa na Imani nao na kutambua kuwa watoto hao tangu sasa watashirikiana katika malezi ikiwa ni sambamba nakujua kila hatua ya ukuaji wake kama watapatwa na Tatizo lolote shirika nalo litawajibika kama mzazi wa mtoto.

 'Kuna watu wanasema vitu vya ajabu kuhusu huduma hii kuwa inataka kuwaingiza watoto sijui freemason au kwneye vitendi vibaya ya maadili jambo ambalo sio kweli,nimekuwa na shirika hili kwa muda mrefu ninajua nini kinafanyika,hivyo niwahakikisshie wazazi ambao watoto wenu wameingia kwenye mradi huu mtanufaika sana na haya maneno hayatakuwepo tena' amesema Isack.

 

Mchungaji Kiongozi wa kanisa la TAG Tandala Jonas Sanga amesema ili kufikia malengo ya mradi huo na kuona tija ni muhimu wazazi kuwalea watoto katika maadili mema kwani malengo ya mradi nikuona watoto wanakua katika maadili mema.

 

'Ndugu zangu malengo ya mradi huu ni kuona mabadiliko kwa watoto wetu hivyo tusaidiane kuwafinyanga hawa watoto kutokaa katika malezi tuliyonayo kuwa katika malezi bora,vinginevyo mradi utakuwa haujasaidia' amesema Mch. Sanga


Mchungaji Sanga na Katibu wa kamati ya mradi huo Peter msigwa wamesema ingekuwa mradi huo una malengo tofauti na misingi ya Imani ya kanisa la Assembles of God TAG wasingekubalina nao.

'Mnajua msimamo wangu kwa wale wanaonifahamu,mnajua msimamo wa kanisa hili na imani yetu,tusingekubali watoto hawa 200 kuwaingiza katika huko wanakosema tusingekubali,lakini niseme kama mtoto wako amesajiliwa hapa basi muwe na amani na sisi watoto wenu wako mikono salama' amesema Peter Msigwa

Kwa upande wa wazazi na walezi Anitha Sanga na Venansia Ngulo wametoa shukrani zao kwa kanisa la TAG na shirika hilo kwa kuwasaidia watoto wao na kwamba fedha mbazo zingetumika kuwahudumia watoto hao sasa watazielekeza katika shughuli nyingine.

'kwa kweli tunashukuru kanisa la TAG na shirika hili kwa kutona maana maisha yetu ni ya kawaida na wakati mwingine watoto wetu wameishia mitaani kwa kushindwa kusomeshwa lakini kwa sasa watasomeshwa tunashukuru sana' wamesema wazazi

Ikumbukwe kuwa watoto 200 kutoka kijiji cha Tandala,Ikonda na ihela wananufaika na mradi huo ambao inaelezwa wasomeshwa,kufadhiliwa matibabu muda wote, na wazazi kuepewa elimu na mafunzo mbalimbali kama ya malezi na ujasiriamali ili wajiinue kiuchumi.

Baada ya kikao wazazi na watoto wakapata chakula kilichoandaliwa na kanisa la TAG Tandala

Wazazi na watoto wakipata chakula cha pamoja baada ya kikao octoba 26.2024











Mratibu wa mradi akitolea ufafanuzi kuhusu makubaliano ya kutoa au kutumia taarifa binafsi katika utekelezaji wa mradi pamoja na kuondoa zuio la kushtakiwa.


Katibu wa kamati ya utekelezaji wa mradi huo kanisa la TAG Tandala akitoa neno katika kikao hicho Peter Msigwa

Mratibu wa Mradi wa CIT kupitia kanisa la TAG Tandala akitoa ufafanuzi wa mradi kwa wazazi na walezi wanaonufaika na mradi huo

Shuhuda na mmoja ya walionufaika na miradi ya Compassion International Tanzania CIT kutoka mkoa wa Iringa ambaye kwa sasa ni mwl wa shule ya sekondari Lupalilo.


Mchungaji Kiongozi wa TAG Tandala akitoa somo kabla ya kuanza kwa kikao

Dua ikifanyika kabla ya kuanza na kumaliza kikao na wazazi wa watoto katika kanisa la TAG octoba 26,2024

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top