Taahadhari Mnyama simba aonekana wilayani Makete tena

Adimin
0

 Mnyama aina ya simba ametajwa kuwepo wilayani Makete mkoani Njombe


Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Maliasili na Mazingira katika Halmashauri ya Wilaya ya Makete Upendo Mgaya katika kikao cha baraza la Madiwani la halmashauri hiyo kilichoketi leo Novemba 7,2024.

Mgaya amesema nyayo za mnyama huyo zimeonekana katika maeneo tofauti ya Kata ya Iwawa hasa maeneo ilipo shule ya msingi St Joakim.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete William Makufwe na Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Hawa Kader wametaka wananchi kuchukua tahadhari juu ya mnyama huyo.

Hii ni mara ya pili kwa kipindi cha miezi miwili tangu kuripotiwa nyayo za mnyama simba katika kata ya Lupila,mbalate na Mang'oto ambaye hata hivyo ilielezwa ameuawa katika wilaya ya Ludewa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top