Baba ajinyonga baada ya kumjeruhi mwanae kwa kitu chenye ncha kali

Adimin
0

Mwanaume Makoye Peter Mayala (45) wa mkoani Shinyanga amejinyonga baada ya kumjeruhi mtoto wake na kitu chenye ncha kali Anna Makoye (06) anayesoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Mwamagunguli.



Tukio hilo limetokea alfajiri ya  Desemba 2, 2024 baada ya marehemu kutokuwa na maelewano na mkewe Elizabeth Mwigulu ndipo mkewe aliamua kukimbia na marehemu kuamua kumjeruhi vibaya mwanaye maeneo ya shingoni na kisha kujinyonga huku chanzo kikiwa bado hakijajulikana.

Jeshi la polisi mkoani shinyanga limefika eneo la tulio kwaajili ya kufanya uchunguzi wa awali na kuzingumza na wananchi wa eneo hilo na kutoa rai kwa wananchi kutojichukulia sheria mkononi pindi wanapokumbana na changamoto za kifamilia.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top