Tembo amuua mwangalizi wake aliyekua akimuogesha

Adimin
0

Tembo amemuua mwanamke mmoja raia wa Uhispania alipokuwa akimwogesha mnyama huyo katika kituo cha tembo nchini Thailand, wamesema polisi wa eneo hilo.

Blanca Ojanguren García, 22, alikuwa akiosha tembo katika Kituo cha Kutunzia Tembo cha Koh Yao, siku ya Ijumaa iliyopita alipouawa kwa kupigwa na pembe za tembo.

Wataalamu wa tembo waliliambia gazeti la lugha ya Kihispania, Clarín kwamba huenda tembo huyo alikuwa na hofu baada kulazimika kutangamana na watalii nje ya makazi yake ya asili.

García, mwanafunzi wa sheria na mahusiano ya kimataifa katika Chuo Kikuu cha Navarra nchini Uhispania, alikuwa akiishi Taiwan kama sehemu ya mpango wa kubadilishana wanafunzi.

Alikuwa katika matembezi nchini Thailand akiwa na mpenzi wake, ambaye alishuhudia shambulio hilo.

Waziri wa mambo ya nje wa Uhispania, Jose Manuel Albares, amesema ubalozi mdogo wa Uhispania huko Bangkok unaisaidia familia ya García.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top