Aziz Ki na Nouma watemwa kikosini

Adimin
0

 Kiungo wa Yanga SC Stephane Aziz Ki na mlinzi wa Simba SC Valentino Nouma wameachwa katika kikosi cha Burkina Faso kilichoitwa leo na kocha Brama Traore kwaajili ya michezo miwili ya kuwania kufuzu kombe la Dunia 2026


Burkina Faso itakuwa nyumbani Machi 16 2025 kucheza mchezo wake wa 5 wa hatua ya makundi dhidi ya Djibouti kabla ya kusafiri kuwafuata Guinea Bissau tarehe 23 Machi 2025

Ikumbukwe kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29 alikuwepo katika kikosi kilichocheza mechi za mwanzoni za michuano hiyo akicheza michezo mitatu na kutoa pasi moja ya goli

The Stallions wanashika nafasi ya 3 katika kundi A ikivuna alama 5 katika michezo minne iliyocheza, nyuma ya Guinea Bissau yenye alama 6 na Misri mwenye alama 10 anayeongoza msimamo wa kundi hilo

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top