Mapya yaibuka mwanamke aliyekaa na mimba miaka minne shinyanga

Adimin
0

 Katika hali isiyo ya kawaida, mwanamke mmoja mkazi wa Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga amebainika kuishi na ujauzito kwa zaidi ya miaka minne kabla ya kufanyiwa upasuaji ambao umebaini kuwa kiumbe aliyekuwa tumboni alikuwa tayari amefariki dunia.


Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 55, alipata ujauzito huo akiwa na miaka 51 na alishindwa kufahamu hali hiyo kwa muda mrefu, jambo lililompelekea kutafuta msaada kwa waganga wa kienyeji akiamini ni matatizo ya kawaida.

 Kwa mujibu wa maelezo yake, alikumbwa na hofu na aibu ya kijamii kutokana na mila na desturi potofu, hali iliyomfanya kukaa kimya kwa muda wote huo.

Baada ya hali yake kuwa mbaya, alifikishwa katika Hospitali ya Manispaa ya Kahama na baadaye kupewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambapo amefanyiwa upasuaji.

Daktari bingwa wa magonjwa ya kina mama na uzazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Augustino Maufi, amesema baada ya vipimo, ilibainika kuwa alikuwa na mimba iliyotunga nje ya mfuko wa uzazi (ectopic pregnancy) hali ambayo kitaalamu ni hatari na huweza kuleta madhara makubwa kwa afya ya mama.

Dkt. Maufi ameongeza kuwa hali hiyo husababishwa na sababu mbalimbali ikiwemo maambukizi kwenye mfumo wa uzazi na kwamba iwapo mama huyo angefika hospitalini mapema, hali hiyo ingaliweza kuzuilika.

Aidha, daktari huyo ametoa wito kwa wanawake wote walioko katika kipindi cha ujauzito kuhakikisha wanapata huduma katika vituo vya afya pindi wanapokumbwa na changamoto yoyote badala ya kutegemea tiba za jadi ambazo mara nyingi huchelewesha au kuzorotesha afya zao.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top