"Tulikosea kweli yule Martha Karua kumrejesha kule, na hili kosa lisitokee tena hapa, hivi mtu anatoka huko analeta ujinga wake hapa halafu eti anarejeshwa mzima, salama salmini kweli. Na yule anayesema anadai kapigwa eti anashuka kwenye gari anajichechemeza kweli? Yule alikuwa apigwe arudi na mitungi ya gesi kule kwao, anapumulia gesi," anaeleza Maryam Omar Said, Mbunge wa Pandani, Zanzibar.
"Tumemuacha Martha Karua anaendelea kuzungumza akiwa Kenya kule, mheshimiwa Waziri hili lisitokee tena. Anayekuja kwetu tunamalizana naye hapa hapa, anayeingia ndani ya kumi na nane zetu, tumalizane naye hapa, hapa," amesema Mbunge Maryam.
FULL VIDEO BOFYA HAPA KUTAZAMA