CHAUMMA Wakomaa na CHADEMA, Ndio adui wao

Adimin
0

 Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amesema licha ya kubezwa na kubeukwa katika harakati zao za kisiasa, sasa wapinzani wao wanalazimika kupambana nao kwa nguvu zote.


Akizungumza wakati wa mikutano ya Oparesheni C4C inayoendelea mkoani Katavi na Tabora, Salum amesema kuwa wapinzani wao wanakaribia kuchoka huku CHAUMMA wakiendelea kuimarika.

"Wametucheka, wametubeza, lakini leo wanapambana na sisi. Tukitoka sisi, wao wanaingia. Tunawaambia wataishiwa mafuta na nguvu. Sisi (CHAUMMA) tunamaliza round hii, tunajaza mafuta, tunaingia round nyingine," amesema.

Ameeleza kuwa helikopta wanayoitumia kwa ziara hizo, baada ya kukamilisha mizunguko ya sasa, itarudi Kenya kwa matengenezo kabla ya kurejea kwa awamu nyingine ya oparesheni hiyo.

"Tunawaambia hiki chombo (helikopta), tunamaliza round hii, kinarudi Kenya kwenda kufanyiwa service, kinarudi, tunarudia round nyingine, halafu ndipo tunaingia tena kwenye kampeni," amesema Mwalimu.

Salum Mwalimu amesema mkakati wa CHAUMMA ni kutumia akili kubwa, busara na hekima kukabiliana na changamoto za kisiasa badala ya kutumia nguvu au ubabe wa maneno.

"Tunahitaji busara kwenye nyakati ngumu, siyo ubabe. Tunahitaji akili kubwa kwenye nyakati ngumu na siyo ubabe. Tumekataa ubabe usioendana na hekima na busara. Unapokuwa na misimamo mikali, lazima uwe na mikakati na akili kubwa ya kutekeleza hiyo misimamo," amesisitiza.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top