Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mary Florian Joachim ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ujumbe wa Chadema, nafasi ambayo ameitumikia kwa takribani miaka kumi na tano sasa.
Katika barua yake ya Juni 02, 2025 aliyoituma kwa Katibu wa Bodi ya wadhamini wa Chadema, Bi Mary ametanabaisha kuwa sababu ya kujiuzulu kwake ni za binafsi, akiamini kwamba kwasasa atashindwa kuitumikia nafasi yake vyema ndani ya Chama hicho Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania.
TAZAMA VIDEO YA LISSU LEO AKIWA KIZIMANI