Watu 10 wauwa na wengine 29 wamejeruhiwa - Shirika la haki za binadamu Kenya

Adimin
0

 Shirika la kutetea haki za binadamu nchini Kenya (KNCHR) limesema kuwa watu 10 wamefariki huku 29 wakijeruhiwa. Watu wawili wamekamatwa na 37 kukamtwa katika kaunti 17.


Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, shirika hilo limesema limeshuhudia kuwekwa kwa vizuizi vya polisi vilivyovuruga matembezi ya watu hususan katika jiji la Nairobi. Vizuizi vingine viliwekwa kwenye kaunti za Kiambuu, Meru , Kisii, Nyeri , Nakuu na Embu, imesema taarifa ya KNCHR.

Shirika hilo la haki za binadamu la Kenya limelaumu ukiukwaji wa polisi wa amri ya Mahakama Kuu inayowataka maafisa wote wanaohusika na udhibiti wa maandamano kuwa wamevalia sare ya polisi, huku likisema limeshuhudia maafisa wa polisi waliovalia sweta zilizofunika nyuso zao(hood), katika maeneo ya Kaunti za Nairobi, Kajiado na Nakuru na Eldoret.

Jijini Nairobi shirika hilo linasema watu waliovalia sweta zenye kofia walionekana kushirikiana na polisi.

Shirika hilo limelaani kushambuliwa kwa ofisi ya haki za binadamu jijini Nairobi na kushambuliwa kwa wafanyakazi wake na raia Jumapili waliokuwa wakiandaa maandamano.

Limeitaka serikali kuacha unyanyasaji dhidi ya mashirika ya kiraia na watetezi wa haki za binadamu.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top