Aliyeiba mafuta lita elfu 35 kisha kuchoma gari adakwa Morogoro

Adimin
0

 Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro limefanikiwa kumkamata Abubakary Mwichangwe (29), Dereva wa lori la mafuta lenye namba za usajili T.661BXW tela namba T.489 BHC ambaye alikuwa anatafutwa Kwa tuhuma za kuiba mafuta aina ya dizeli lita elfu 35 yenye thamani zaidi ya Tsh. milioni 77 kisha kulichoma moto gari hilo kwa lengo kupoteza ushahidi na yeye akatokomea kusikojulikana.


Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro SACPnAlex Mkama amesema tukio hilo limetokea March 16,2025 katika Kijiji cha Msimba Wilaya kilosa Mkoani Morogoro barabara ya Morogoro - Iringa.

RPC Mkama amesema Mtuhumiwa aliiba mafuta kwa kula njama na Mameneja wa vituo vya mafuta kisha alipofika katika Kijiji cha Msimba aliliangusha gari korongoni na kujaribu kulichoma moto kabla ya Wasamaria wema kufika na kuzima na baada ya tukio Dereva alikimbia kusikojulika hadi baadaye Polisi walipomkamata ambapo Polisi haijasema imemkamata akiwa wapi kwasababu za kiupelelezi kwakuwa bado wengine aliokula nao njama kuchoma gari wanaendelea kusakwa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Idawa Media Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top