Yanga wasema NO REFOMS NO DERBY, Watoa Tuhuma Nzito kwa Kigogo wa serikali

Adimin
0
 

MSEMAJI wa Yanga, Ally Kamwe amesema klabu hiyo, iko siriazi katika msimamo wa kutocheza mechi ya Kariakoo Dabi dhidi ya Simba, akisema Bodi ya Ligi Tanzania imepotosha juu ya matakwa yao manne.

Akizungumza jioni hii katika makao makuu ya Yanga, Kamwe amesema Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi Almas Kasongo ameshindwa kufafanua vizuri matakwa manne kwamba yapo ya muda mfupi na muda mrefu.

Kamwe amesema matakwa ya muda mfupi ni pamoja na kuvunjwa kwa Kamati ya Usimamizi ya Ligi kwa kile ilichodai imeshindwa kusimamia kwa weledi usimamizi wa Ligi kwa msimu wa 2024/25

Amesema takwa la pili la muda mfupi ambalo linakwenda sambamba ni kujiuzulu kwa Kasongo alipotosha Bodi wakati wa kuahirishwa kwa mchezo namba 184 uliopangwa kufanyika Machi 8, 2025.

"Jambo lingine la muda mfupi ni kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao, wote mnajua kumekuwa na vilio vingi juu ya maamuzi ya waamuzi, waamuzi wanafanya makosa na bado wanapewa mechi za kuamua ," amesema Kamwe.

"Kama hamfahamu hii Kamati ya waamuzi ipo chini ya Katibu Mkuu wa TFF kwa kuwa matatizo yamekuwa mengi Yanga tunasema na yeye atupishe.

Aidha, Kamwe amesema takwa la kuunda Bodi huru ndio jambo la muda mrefu ambalo wamewaachia TFF na Bodi kulifanyia kazi ambapo endapo halitafanyiwa kazi kwa uzito wanaweza wasishiriki Ligi msimu ujao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top